Friday, January 1, 2010

HAPPY NEW YEAR FROM AY


Mwanamuziki Ambwene Yessayah au maarufu kama AY,anakusalimia na kukutakia Kheri ya Mwaka Mpya! Ametuagiza tufikishe ujumbe na sisi bila kinyongo na kwa sababu ni wajibu wetu kukupa habari tunawasilisha.

Yeye mwenyewe yuko wapi? AY yupo nchini Rwanda katika jiji la Kigali.Hapo ndipo atakapoukaribishia mwaka mpya. Anasema show ya kwanza anaifanya usiku wa leo,yaani mkesha wa mwaka mpya ndani ya Top Tower Hotel na kesho anatarajia kuuanza mwaka mpya pale katika Uwanja wa Amahoro.

Katika maonyesho hayo,AY ataperform na wasanii wengine kutoka Afrika Mashariki kama vile Farias(Burundi),Amani(Kenya),HB Toxic(Uganda),K8(Rwanda) na wengine wengi.Nchini Rwanda,AY ameongozana na Producer wake Hermy B.

Kila la kheri AY.



Share/Save/Bookmark

No comments:

Post a Comment

 

.